EPHRAIM SEKELETI-EASTER CONCERT 2012 - BY MSAMA PROMOTION

Monday, July 23, 2012

JAMES TEMU (UNCLE JIMMY), BAHATI BUKUKU, RULEA SANGA (BLOGER), DAVID ROBERT NA WENGINE KUJA NA FILAMU KALI YA KUMTUKUZA MUNGU WETU "DUNIA HAINA HURUMA"

Mwandishi: Rulea Sanga

Mshiriki mwingine wa filamu ya "Dunia haina Huruma", Blogger wa RUMA AFRIKA, Rulea Sanga. Hapa akiwa katika gari la Wise Men wa Nabii TB Joshua katika Synagogue ya THE SCOAN. Kumbuka mwezi Aprili 2012 aliitwa na Nabii TB Joshua kutokana na kazi yake nzuri ya blogu yake ya www.rumaafrica.blogspot.com

Umefika wakati Mungu amezungumza na hawa watumishi wa Mungu kwa kuwapa maono ya kutengeneza filamu ya "Dunia Haina Huruma". Ujumbe huu unatoka katika nyimbo mpya ya mwimbaji maarufu Tanzania, Bahati Bukuku inayoitwa "Dunia haina Huruma" Nyimbo hii imekuwa gumzo jijini Dar es Salaam kutokana na ujumbe wake unaogusa maisha ya watu na kukuweka karibu sana na Mungu unapousikia. Kama hujawahi kuusikia, nakuomba ujitahidi kusikiliza Praise Power Radio na Wapo Radio utabarikiwa.

Mhusikaka mkuu wa filamu hii, Bahati Bukuku

Kutoka na wimbo huu, watumishi wa Mungu wameamua kukaa chini na kuuzambaza ujumbe huu kwa njia ya filamu. Kwahiyo utafaidika kuusikia kwa njia ya uimbaji na pia kwa njia ya maigizo.

Katika filamu hii kutakuwa na watumishi wa Mungu kama James Temu a.k.a Uncle Jimmy (ambaye ni mwigizaji wa filamu Tanzania na ni mtangazaji wa Praise Power Radio Tanzania, mbali na hapo ni blogger) , Rulea Sanga (ambaye ni blogger na ni graphic designer, na mwezi April 2012 alibahatika kuitwa na Nabii TB Joshua kutokana na kazii yake nzuri ya blogu), David Robert (huyu ni muimbaji wa nyimbo za injili Tanzania na ni mjasiliamali mkubwa sana Tanzania), Bahati Bukuku (Huyu ndiye mhusika mkuu wa filamu hii, ni mwimbaji wa nyombo za injili Tanzania na amekuwa baraka kwa wale waliosikia nyimbo zake), Riyama Ally (huyu ni mwigizaji wa filamu Tanzania, amefanya kazi nyingi katika uigizaji)

Wimbo wa Bahati Bukuku wa Dunia haina huruma unagusa sana mioyo ya watu, hasa wale walioko katika ndoa na wale wanaotaka kuingia katika ufalme wa ndoa. Kutokana na wimbo huo, mtumishi wa Mungu Bahati Bukuku akaamua kuja na wazo la kutengeneza filamu ambayo itaonyesha kila kitu alichokiimba katika wimbo huo.

Mshiriki mwingine wa filamu ya "Dunia haina Huruma", Blogger wa RUMA AFRIKA, Rulea Sanga. Hapa akiwa katika gari la Wise Men wa Nabii TB Joshua katika Synagogue ya THE SCOAN. Kumbuka mwezi Aprili 2012 aliitwa na Nabii TB Joshua kutokana na kazi yake nzuri ya blogu yake ya www.rumaafrica.blogspot.com

Kwa sasa kila kitu kuhusina na filamu hii kimeandaliwa, ila kilichobaki ni kumtafuta dada mrembo na mwenye kuvutia, kwani kuna sehemu inahitajika kwaajili ya dada ambaye ni mrembo sana. Kama wewe unajiona ni mrembo na uunajiamini na unaweza kuigiza tunaomba uwasiliane kwa namba hii +255 713-763939.


Kumbukeni haya yote yanafanyika kwaajili ya kumtangaza Kristo na kuonyesha kuwa hata sisi tuliokoka tunaweza kufanya vitu vikali na vizuri. Umefika wakati wa kupenda vilivyo vya Mungu na ku-support kazi ya Mungu. Support yako itatuwezesha kufanya vitu vikali. Mungu anatumia watu kufanikisha kile anachotaka kifanyike, na leo wewe utakuwa ni mmoja wa wale Mungu anapenda ushiriki katika ku-support kazi hii isonge mbele. Kama unamchango wako wowote tutashukuru sana kusikia na kupokea kwako, mchango unaweza ukawa na mawazo, fedha au vitu. Kama wewe ni mmiliki wa vyombo vya shooting unaweza ukajitokeza tukafanya kazi ya Mungu.

Kwa mujibu wa Bahati Bukuku, amesema filamu hii itakuwa ya utofauti na filamu za watu wengine kwani watu watakao shiriki filamu hii watapimwa uwezo wao wakufanya kazi napia watasafiri baadhi ya mikoa kukamilisha kusudio la filamu hii.
Wadau wa blogu hii endeleni kuitembelea, ili mfahamu kitu kinachoendelea.

Riyama Ally ni mtumishi wa Mungu na anacheza filamu za Kitanzania (Bongo Movie). Naye atashiriki katika filamu hii.

David Robert, ni mwimbaji wa nyimbo za injili Tanzania na mjasiliamali. Atashiriki
Uncle Jimmy , ni mwigizaji katika Bongo Movie na amecheza na waigizaji wakubwa Tanzania akiwaomo Ray, JB,O na wengine wengi. Katika filamu hii utaona kazi yake ya uigizaji katika muonekano mwingine.


NIKUPE KIONJO CHA TAMTHILIA

Bahati Bukuku alipigiwa simu na mwanamke mmoja ambaye alijitambuliha kuwa yeye ni mke mwenzake, alimpa taarifa mbaya akimwambia "Nenda kachukue mzoga wako Muhimbili" . Bahati Bukuku akiwa katika kutafuta marafiki zake kuulizia taarifa hizi ili kujua zaidi, aliamua kufika mochwari Muhimbili, na alipofika Muhimbili alikutana na taarifa mbaya za kuumiza moyo wake kutoka kwa wale waliokuwa hapo Muhimbili.
Bahati Bukuku aliingia chumba cha maututi na kuona mpenzi wake amepoteza fahamu na hawezi kumtazama. Nilijisemesha kuwa "Dunia haina huruma, haina fadhili, nani mwenye huruma anifariji, moyo unavuja damu kwa matatizo ninayopata."
Bahati Bukuku akamua kuwapigia ndugu wa mume wake Mbeya ili awaeleze yaliyomsibu, lakini cha kushangaza ni kwamba wote walimsusia. Akajaribu kuchukua kitabu cha Bank ili kuangalia kama kuna pesa kidogo zimsaidie, lakina cha kusikitisha anaona ATM haizomi nikimaanisha hakuna pesa. Hakuchoka akaenda kwa daktari na kutaka kumuuzia gari aina ya Vogi, lakini daktari anakataa na kusema haya magari yanakula mafuta sana kwahiyo sitoweza kuwa nalo. Akiangalia marafiki zake wanazidi kularua moyo wake kwa maneno makali.
Bahati Bukuku kila akimwaangalia mume wake anazidi kuchanganyikiwa na hawezi kuongea naye. Mashemeji zake hawataki kusaidia na kila akiomba msaada kutoka kwao, nao wanamwambia "Shemeji sisi tunaenda kuangalia mpira Ulaya" akiwaambia mawifi zake nao wanamwambia, "Wifi hatuwezi kukusaidia, tunaenda kucheza segere".
Bahati Bukuku akaamua kwenda tena kwa daktari kuomba asaidiwe. Na chanzo cha matatizo kikaanza hapo. Bahati akibdi azae na huyu daktari ili apate msaada, maana amehangaika sana bila ya kupata msaada, na mgonjwa hali yake ni mbaya sana.

Mzigo ukazidi kwa Bahati Bukuku, hali ikazidi kuwa mbaya sana, maana amefanya kosa la kufanya tendo la ndoa na daktari na kuzaa mtoto, na bado ndugu hawampendi.
Baada ya kupata nafuu kwa mgonjwa na kurusiwa nyumbani na kuendelea na maisha yake ya kwaida, Bahati Bukuku akamwambia kuwa nimezaa na daktari. Na hii nililifanya kutokana na kushindwa kupata msaada kutoka kwa ndugu na marafiki, wote walinikimbia, kwahiyo nikaamua kufanya hivyo kwa daktari ili nipate pesa ya kukusaidia upate matibabu.

Mume na Bahati Bukuku aliposikia habari hizo kuwa mke wake ana mtoto na daktari akachukua mapnga na kutaka kumuua.

Mume na Bahati aliondoka na baadae Bahati Bukuku akaitwa kijijini kwa mume wake. Alipofika kijijini akawasalimia, nao hawakuta kumjibu wala kumsikia. Kikao kikakaa kutaka kumhukumu, na wakamwambia Bahati Bukuku, "Kama unataka kuishi katika familia hii, mtoto auawe". Akamtazama mume wake na yeye akamtazama kwa hasira. Bahati aakjiuliza, amkimbile nani kwani ndugu, marafiki na mume wake hawamtaki.
Ndugu wakmuweka mtoto kati ili wampige mapanga, akatokea baba mmoja na kuwauliza, ambaye hana dhambi na awe wa kwanza kupiga panga huyu mtoto. Mume na Bahati Bukuku baada ya kusikia hilo aliomba msamaha kwa mke wake na kusema kuanzia leo hii ya dunia yameisha nataka kutengeneza na Mungu.

Bahati amegundua ya kuwa Mungu anaweza kujibu maombi na kusamehe. Hii ni stori fupi ya tamdhilia ambayo itakujia kwako, kuna mengi ambayo utayaona katika filamu hiyo, Utaona mazingira yatakyotumika, wahusika wanatavyokuwa serious kukuletea huu ujumbe.

Lakini nataka kukuuliza wewe mdau wangu, unafikiri Rulea Sanga, David Robert, Uncle Jimmy, Bahati Bukuku n, Riyama Ally anaweza kufaa katika kitengo kipi?

Kwa haraka haraka kuna wahusika wafuatao:

1. Mke wa yule mume mgonjwa
2. Mume ambaye ni mgonjwa
3. Dada aliyempigia simu mke wa yule mume
4. Marafiki /mashoga wa mke wa mume
5.Daktari
6. Ndugu wa mume
7. Watu waliokataa kumsaidia Bukuku akiwa na shida.
8. Ndugu aliyepigiwa simu na Bahati Bukuku
9. Wacheza segere
9. Ndugu waliomua kwenda Ulaya kuangalia mpira
10. Mtoto wa daktari ambaye aliambiwa akatwe mapanga
11. Mtu aliyewambia wasimkate mapanga
TUNAOMBA MAONI YAKO.

FILAMU YA "SIKU YA MWISHO-666" KUWA SOKONI WIKI HII

Source: Ruma Africa & Papa Sam

(Kuhusiana na habari zingine kuhusiana na hii filamu tembelea www.rumaafrica.blogspot.com na www.samsasali.blogspot.com. Tutatakuwa tunakuletea kinachoendelea)

Ile Filamu ambayo inasubiriwa kwa hamu kubwa hususani Jamii Ya Kikristo Ya Siku za Mwisho inakamilika wiki hii na Kabla ya Kuingia Sokoni Mapema Mwezi Ujao.
Katika Filamu hiyo ya kibongo ambayo Papaa Ze Blogger amecheza kama Apostle P Nizo, ambaye ni Mtume na Nabii mwenye Kanisa lenye Ishara na Miujiza mingi na Baraka kadha wa Kadha pasipo waumini wa Kanisa hilo kutambua kuwa Apostle Nizo ana "Source Of Power" isiyotoka Juu.
Filamu hiyo yenye maudhui ya Kuwakumbusha Wakristo kuhusu Siku Za Mwisho na Kurudi Kwa Yesu Kristo imesheheni Vipaji Lukuki Vya Wakristo Katika kufikisha Ujumbe kwa Jamii.

Hapa ndipo Wanapokuwa kwenye Ibada Zao Wakisali ...Its a Nice Scene

Kushoto kabisa ni Papaa Ze Blogger akicheza Kama Apostle ndani ya Scene hiyo akiwa amevaa tofauti na wengine sababu na nafasi yake katika Impact katika Jamii

Hapa Apostle Nizo Akiwa anafatilia Ibada kwa Unakini Mkubwa ndani ya Chumba Cha Siri

Hapa Papaa Ze Blogger akiecheza Kama Apostle P, akidaka "power'
Apostle P Nizo akiwa na Kisu tayari kwa Ibada Ya Sadaka....Its very interesting Scene

Wakuu Katika Katika Kujipanga Kimkakati Mara baada ya Ibada ya Chumba Cha Siri

Kulia ni Papaa Ze Blogger ambaye amecheza kama Anointed Apostle, Katikati ni Pastor Alex, ambaye amecheza kama Mfanyabiashara mkubwa ambaye pia ni Mzee wa Kanisa Wa Apostle Nizo, na Kushoto Ni Mwanadada amecheza kama Mwanaharakati wa Haki za Wanawake na Mjasiriamali ambaye yuko connected na "chumba cha siri'

Laurence akiwa mwenzake ambaye wamecheza kama Askari wanaokagua magari kama yana sticker ya 666 maana hutaweza nunua mafuta wala kuendesha gari kama haijagongwa 666.

Hawa Watu Watatu wametisha Sana katika Scene hii ya "Chumba Cha Siri" Mpaka Pastor Kaduma Mtunzi wa Filamu hiyo, na Director Wa Filamu hiyo Mr. Mtitu Wakapiga picha na Jamaa

Scene hii Jamaa akiwa ameandaa Part nyumbani kwake ambapo amealika ndugu jamaa na marafiki,

Wageni Waalikwa Mabibi na Mabwana wakifurahia Chakula nyumbani kwa Mtumishi ambaye baadae atabaki sababu kumbe alidai amebarikiwa na mungu kupata hela kumbe Kapiga EPA.
Shemeji Yangu Edna Luvanda akiwa ndani ya Scene ya Siku za Mwisho, Kulia ni Dorcas Sakani ndani ya Filamu.

Full Kula
Hapa Madaktari wakijiandaa ndani ya chumba Cha Operation kwa ajili ya kumuhudumia mgonjwa

Hapa Wakiendelea na Operation

Kazi Ikaendelea
 
Daktari Bingwa akiwa Kazini kwenye Scene

Wakiwa Ndani ya Chumba Cha Operation Yesu anarudi na Daktari Bingwa anatwaliwa, sokomoko waliobaki ndani ya Chumba Wamuhudumie Mgonjwa ama Wamtafute Dr. Bingwa waliyetwaliwa.

Wednesday, June 13, 2012

MPIGIE KURA CHRISTINA SHUSHO, IPIGIE KURA TANZANIA, IINUE AFRICA
VIVA SHUSHO....VIVA TANZANIA
Christina Shusho,akihojiana na mablogaz wa Kitanzania katika hotel ya The Atriums iliyoko Sinza Africa sana
Siku ya jana jioni mablogaz wanaomiliki blogu za Kikristo Tanzania, Rulea Sanga, Uncle Jimmy, Sam Sasali, K-Junior, Martin Macele walikuwa na mahojiano na Christina Shusho katika hotel ya The Atriums Sinza Africasana kuhusiana na shindano kubwa lililoko machochoni pa mtumishi wa Mungu Christina Shusho.

Christina Shusho alimshukuru Mungu kwa kuweza kumtumia kama chombo kufikisha ujumbe kwa jamii kwa njia ya uimbaji na pia kuweza kushiriki katika Gospel Music Awards Africa. Pia aliwashukuru mablogaz kwa kazi yao nzito wanayofanya kumtangaza katika blogs zao na kupoteza muda wao kwaajili ya kumuinua Kristo.
Aliwaomba Watanzania na Africa nzima kumchangua Christina Shusho ili kuliwakilisha Bara la Africa,Tanzania na kumuweka Kristo juu ya vyote.
Christina Shusho ni mwimbaji wa nyimbo za Injili Tanzania na amekuwa chachu kwa waimbaji wenzake na kwa watanzania kwa uimbaji wake na ujumbe naoutoa ambao umekuwa na mguso katika kukarabati imani za watu.
Christina Shusho anategemea ku-perform DAR LIVE siku ya jumapili, kwahiyo amewaomba Watanzania wote kufika mahali pale na kuweza kumpigia kura, kutakuwepo na mablogaz na kompyuta zao ambapo utakutana nao na watakuelekeza jinsi ya kupiga kura....

Tukutane Jumapili Dar Live
1.Emmy Kosgei-Kenya
2.Dena Mwana – Congo
3.Ntokozo Mbambo- South Africa
4.Rebecca- UK
5.Gifty Osei- Ghana
6.Kefee -Nigeria
7.Onos Ariyo- Nigeria
8.Diana Hamilton-UK
9.Christina Shusho -Tanzania
10.Lara George- Nigeria
VIVA SHUSHO, VIVA TANZANIA-MSIKILZE SHUSHO ALIPOKUWA ANAONGEA NA MABLOGAZ JANA THE ATRIUMS HOTEL SINZA AFRIKASANA
USIKOSE MTUMISHI WA MUNGU...NJOO TUFANYE KAZI YA BWANA KWA KUM-SUPPORT MTANZANIA MWENZETU 

KAMA ULIKUWA HUJUI KUHUSIANA NA MASHINDANO HAYA, TAFADHALI SOMA HAPO CHINI



Siku 18 zimebakia kabla ya pazia la upigaji kura kufungwa kwa waimbaji wa gospel barani Afrika, ambao wanawania tuzo mbalimbali kupitia Africa gospel music awards ambazo zinatarajiwa kutolewa siku ya jumamosi ya tarehe 7 mwezi wa 7 mwaka huu huko jijini London nchini Uingereza. Ambapo kama ilivyokuwa kwa mwaka jana mwimbaji wetu mmoja tu, ametutoa kimasomaso kwa kupendekezwa katika kuwania kupata tuzo hizo mwimbaji huyo si mwingine bali ni Christina Shusho, ambaye mwaka jana alitoka mikono mitupu lakini mwaka huu tukiungana kwa pamoja watanzania wote kwa kumpigia kura lazima atarudi na tuzo zote mbili alizopendekezwa kuwania.

Shusho yumo kwenye kuwania mwimbaji bora wa kike wa mwaka pamoja na mwimbaji bora wa mwaka Afrika ya mashariki, tuzo ambazo anawania na waimbaji wengine wanaofanya vyema kwenye gospel barani Afrika wakiwemo wakina Ntokozo Mbambo wa Afrika ya kusini na waimbaji wengine. Kikubwa ninachoweza kukwambia tukifanikiwa kuunganisha nguvu zetu kwa pamoja kwa kumpigia kura atakuwa nanafasi kubwa ya kutwaa tuzo hizo, kwasababu waimbaji wengine wanaowania tuzo hizo wengi wao wanatoka nchi moja hali ambayo itafanya kura zao kugawana kitu ambacho kitatupa nguvu ya kumwezesha Shusho kurudi na tuzo kwani Tanzania nzima kura zetu tunaelekeza kwake.

Mikakati mbalimbali inafanywa ili kuhakikisha kila mtu anashiriki katika upigaji kura kwakuwa hauhitaji kulipa ili kupiga kura, kikubwa unatakiwa ujiandikishe kwenye tovuti ya shindano hilo ambayo maelekezo yake yapo chini ya habari hii, zaidi kama nilivyoandika mikakati inafanywa ili kuhakikisha watanzania wanashiriki kikamilifu katika zoezi hili katika siku 18 zilizobaki. Hapo jana bloggers walikutana na Christina Shusho katika hoteli ya Atriums iliyopo Sinza jijini Dar es salaam ili kupanga mikakati zaidi ya kuweza kupata tuzo hizo ambazo faida yake ni kumwinua Yesu pamoja na kuitangaza nchi yetu ya Tanzania duniani. Natumai umenielewa ili kupiga kura ingia kwenye link hii na kufuata maelekezo chini yake.
http://www.africagospelawards.com/nominate.html


AGMA 2012 VOTING GUIDELINES
1. Click on the 'VOTE NOW' button.
2. Register your email address, confirm and submit.
3. Check your email (inbox) and you will find the link to vote.
4. If you do not find the link in your email inbox, please check your junk mail folder.
5. Once you have connected to the voting page please make your selections and submit (you can only vote for one nominee from each category).
6. You do not have to vote in every category.


ANGALIA BAADHI YA PICHA ZA BLOGGERS NA CHRISTINA SHUSHO HAPO JANA 
Kikao kikiendelea

Blogger Victor kulia akinukuu jambo kutoka kwa Christina Shusho
Rulea Sanga alipoamua kupiga picha ya pamoja
Shusho akieleza jambo kwa mabloggers
 Victor akizidi kuchangia nawazo yake
K-Junior akiwa busy na kuchukua maphotoz

Watumishi wa Mungu wakihakikisha kila kitu kinaenda sawa


Papaa akimuelezea Shusho mikakati ya mabloggerz kuhusiana na upigaji kura


Kutoka kulia ni Shusho, Martin Malecela pamoja na Victor Mboya wakimsikiliza Rulea Sanga akimpongeza Shusho kwa juhudi zake


Rulea Sanga akisikiliza kwa makini mchakato wa kupata tuzo ulivyo.


Mablogaz  na mchungaji aliyoko upande wa kulia


K-junior wa kwanza upande wa kulia akimsikiliza mchungaji wa Vijana


Hakika kikao kilinoga wajameni.

Unclejimmy


Kikako kikiendelea na mabloggerz Tanzania waliojikita kumtangaza Kristo

''Inuka maana shughuli hii yakuhusu wewe, uwe na moyo mkuu, ukaitende (Ezra 10;4)''.
VIVA SHUSHO, VIVA TANZANIA.

Sunday, May 13, 2012




BLOGGER WENU, RULEA SANGA NINGEPENDA TUSHIRIKIANE KULA HIKI CHAKULA NILICHOPATA KWA NABII TB JOSHUA NILIPOPATA MUALIKO WA KUMTEMBELEA NIGERIA-LAGOS APRIL 2012

UNAWEZA KUNUNUA HIKI KITABU KINACHOITWA "THE MIRROR PROPHET TB JOSHUA"

Posted by Rulea Sanga +255 715 85 15 23 |  www. rumaafrica.blogspot.com 

GET THIS BOOK-"THE MIRROR PROPHET TB JOSHUA"
Through this book you will learn a lot of things.

As your blogger, Rulea Sanga I'll be giving you some few points of the Word of God from TB Joshua's Book:
Today we shall see DANIEL
Prophet TB Joshua 

DANIEL trial did not make him lose faith in God, rather it made him pray the more.
Daniel 6:1-28

Daniel was a man of prayer, that was why made the decree. Daniel was still praying because he knew His God was the God that saves and rescue.

Before you can show your faith, you must know your God as One that saves and rescues; you must know what you need to be. Before you can have faith in you God, you must first believe in Him alone and then trust in Him alone. You don't need to support God to do His work. Our duty is to have faith in His finished works.

Daniel's experience of hard time was to be in the lion's den.

We should trust in God in every trial. In hour of adversity, we should trust in God. For the reasons that Daniel trusted in God in the hour of adversity.

God became known all over, all the earth trembled before his God was known as God who rescues and delivers.

Today, christians believe in God but not in the times of trial. 

The believe only when everything is going fine, and everyone is speaking well of them. When you are afraid,  your god will be a god of fear. When you are doubt during you crisis, your god will be a god of doubts. However, when you believe in God in your crisis, your God will be the God of rescues.
Rulea  Inside SCOAN Synagogue

What made Daniel Stronger:
1. His status was elevated
2. He began to dine with kings and men of substance: King Darius began to recognize him.
3. His faith became a state one: the whole country said, "the God of Daniel everybody should worship, obey and respect!"
4. His relationship with God shifted to another level.

TALK WHAT YOU BELIEVE
WORDS TO MEDITATE ON DAY AND NIGHT.
MEDITATION BRINGS REVELATION.

Daniel 5:14-15
"A man of faith is led by an indwelling Spirit of grace, which is greater than he would dwell in the world"

Daniel 6:26-27
"Before you can show your faith you must know that God is the God that saves and rescue"
 Rulea Sanga Outside SCOAN Synagogue

We shall continuel next time

Copied by Rulea Sanga from the Book of TB Joshua

Monday, May 7, 2012


"GET TOGETHER PARTY" KUFANA LEO KATIKA  HOTELI YA ERICK SHIGONGO -"THE ATRIUMS"- SINZA AFRIKASANA-DAR

KIKAO CHA MALIZIKA JANA KUHUSU "PARTY YA GETHER TOGETHER"
Kutakuwa hakuna kiingilio kwa kila mtu atayefika mahali pale. Hii ni party inayowashirikisha watu wote wanaompenda Mungu na kutakuwa na uimbaji kutoka kwa waimbaji wa injili mbalimbali. 

Utapata muda wa kuonana na waimbaji wa nyimbo za injili, maproducer, mabloggers, watangazaji wa radio za injili, wachekeshaji, wajasiliamali, baadhi ya wachungaji. Mbali na kuona utwasikia nini wanakifanya katika sekta zao.

Pia kutakuwa na "SURPICE" ambayo itakufanya ubaki mdomo wazi na kutosahau hicho kitu kitakachotokea mahali hapo siku ya leo.

Party itaanza saa 12:00 jioni na hakuna kiingilio. Utapata chakula cha kutosha kutoka kwa wahudumu wa "The Atriums Hotel" kwa bei nafuu sana.

Party itakuwezesha wewe kufahamiana na watu na kuwezesha wewe kupata "Connection" na watu ambao ulikuwa huwajui. Kumbuka kuja na business card yako kwaajili ya kugawa mawasiliano kwa yule utayekutana naye.

Mimi nikutakie siku njema na usikose kuja na ngugu na jamaa zako !!!!!!!!

 Kamati ya maandalizi: Erick Brighton, Rulea Sanga, Lister, Kisaka, Noel Tenga, Boniface Magupa, Makondeko




Blogger, Rulea Sanga akitokelezea katika kikao